Julius K. Nyerere

Julius Kambarage Nyerere was the first prime minister of independent Tanganyika (1961) and later became the first president of the new state of Tanzania (From 1964 to 1985). Among many other things, he is remembered for his introduction of the Arusha Declaration on Socialism and Self-Reliance.

Books by Julius K. Nyerere

3 Books found
Insha Tatu za Kifalsafa

Authors: Julius K. Nyerere

In Occasional Papers

By OLS Admin

Hazina kama hii ya mawazo, fikra na maandishi mahiri ya Mwalimu katika insha, yenye ladha ya kipekee ni nadra sana kupatikana kutoka kwa wanasiasa wa kisasa. Tuna imani kwamba mbali ya kufarijika, kizazi hiki na vizazi vijavyo vitakuwa warithi waaminifu, waadilifu na wabunifu wa lulu hii ya ufahamu na usomi.

Azimio la Arusha: Majibu kwa Maswali

Authors: Julius K. Nyerere

In Occasional Papers

By OLS Admin

Katika kuitikia tangazo la Azimio la Arusha, wabunge waliwasilisha takriban maswali 21 kuhusiana na Azimio hilo ambayo yalijibiwa na Mwalimu Nyerere mwenyewe kama ilivyo katika kijitabu hiki. Madhumuni ya kuchapisha kijitabu hiki ni kuwakumbusha vijana wetu historia ya Azimio na kuibua mjadala kuhusu mazingira ya leo na somo gani tunaweza kujifunza.

  • Featured
Tukate Mirija ya Unyonyaji

Authors: Julius K. Nyerere

In Kutoka Kavazini

By OLS Admin

Hotuba hii ya Mwalimu, aliyoitoa nusu karne iliyopita, inatoa nafasi nyingine ya kutufikirisha na kutuongoza kila tutakapokuwa tunatafakari jinsi ya kuendeleza ukombozi wa wavujajasho kwa kutumia itikadi na nadharia ya kimapinduzi. Aidha, hotuba hii inatuelekeza jinsi ya kupanga mikakati ya kimapinduzi kwa sababu mapinduzi, hususan mapambano dhidi ya ubeberu na vibaraka wake, sio lelemama na hayaji kwa kulalama.