eBooks

14 Books found
  • Featured
Uanazuoni wa Mwalimu Nyerere

Authors: Bashiru Ally , Saida Yahya-Othman

In Occasional Papers

By OLS Admin

Katika kitabu hiki, waandishi wanamuelezea Mwalimu kama mwanafalsafa, mwanazuoni, mshairi na pia mmajumui wa Kiafrika. Kupitia kitabu hiki, ambacho kimeandikwa kwa lugha nyepesi ya Kiswahili, watafiti, wanazuoni na wasomaji kutoka makundi mbalimbali ya jamii yetu watapata nafasi ya kuelewa kwa undani misingi ya misimamo ya Mwalimu.

    Uchumi wa Viwanda na Uchumi wa Kitaifa

    Authors: Ng’wanza Kamata

    In Kutoka Kavazini

    By OLS Admin

    Kijitabu hiki kina nyaraka mbalimbali zikiwemo hotuba za Mwalimu Nyerere zinazojadili mafanikio na matatizo ya kujenga viwanda baada ya uhuru na baada ya Azimio la Arusha. Tuzisome kwa makini, tuzitafakari hoja mbali mbali zilizomo humu katika muktadha huu mpya wa nchi yetu na hali ya dunia ilivyo sasa.

    • Featured
    Higher Education and Africa’s Development Agenda

    Authors: Paul Tiyambe Zeleza

    In Nyerere Dialogue Lecture

    By OLS Admin

    This Lecture by Professor Paul Zeleza astutely traces the development of higher education in Africa and globally in its various dimensions. It articulates the major concern of most educationists, which is the commercialisation, vocationalisation, disarticulation and direct or indirect privatisation of higher education, particularly university education.

    • Featured
    Tukate Mirija ya Unyonyaji

    Authors: Julius K. Nyerere

    In Kutoka Kavazini

    By OLS Admin

    Hotuba hii ya Mwalimu, aliyoitoa nusu karne iliyopita, inatoa nafasi nyingine ya kutufikirisha na kutuongoza kila tutakapokuwa tunatafakari jinsi ya kuendeleza ukombozi wa wavujajasho kwa kutumia itikadi na nadharia ya kimapinduzi. Aidha, hotuba hii inatuelekeza jinsi ya kupanga mikakati ya kimapinduzi kwa sababu mapinduzi, hususan mapambano dhidi ya ubeberu na vibaraka wake, sio lelemama na hayaji kwa kulalama.

      Towards Feminist Pan-Africanism and Pan-African Feminism

      Authors: Sylvia Tamale

      In Nyerere Dialogue Lecture

      By OLS Admin

      In this magnificent lecture Professor Sylvia Tamale of the School of Law, Makerere University, adroitly lays bare one of the appalling silences in the history of Pan-Africanist and nationalist ideas. She does not simply and mechanically transpose it to her story. Through research and analysis, she demonstrates the central role played by women in the very origin and development of Pan-Africanism.

        Simulizi za Azimio la Arusha

        Authors: Prof. Issa Shivji , Bashiru Ally

        In Special Publications

        By OLS Admin

        Simulizi za Azimio la Arusha ni chapisho maalum la Kavazi la Mwalimu Nyerere liloandaliwa kwa ajili ya maadhimisho ya miaka hamsini ya kuzaliwa kwa Azimio. Simulizi hizi zinachambua, kwa muhtasari, mpangilio wa Azimio na misingi yake kwa mtazamo wa kifalsafa na kiitikadi na hotuba ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa katika semina ya wakuu wa serikali.

        • Featured
        Mwalimu Nyerere: Pan African Nationalist

        Authors: Ng’wanza Kamata

        In Nyerere Dialogue Lecture

        By OLS Admin

        This, Ng’wanza Kamata’s lecture, titled Mwalimu Nyerere: Pan African Nationalist or Nationalist Pan African? was delivered in November 2015. In this lecture, he traces and compares the origins of Nkrumah’s and Nyerere’s Pan-African thought, his main thesis being that whereas Nkrumah arrived at territorial nationalism via Pan-Africanism, Nyerere’s Pan-Africanism was through territorial nationalism.

          Mazungumzo na "Kingunge" wa Itikadi ya Ujamaa

          Authors: Prof. Issa Shivji

          In Kutoka Kavazini

          By OLS Admin

          Kitabu hiki kimebeba mazungumzo aliyofanya Profesa Issa Shivji na hayati Mzee Ngombale kwa wakati na madhumuni tofauti. Kutokana na umuhimu wake wa kipekee, Kavazi la Mwalimu Nyerere limeona ni sehemu ya jukumu lake kuchapisha na kuiwekea rekodi ya kudumu ya mchango wa mwanasiasa na mwanazuoni wetu mahiri, Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru.

            Azimio la Arusha: Majibu kwa Maswali

            Authors: Julius K. Nyerere

            In Occasional Papers

            By OLS Admin

            Katika kuitikia tangazo la Azimio la Arusha, wabunge waliwasilisha takriban maswali 21 kuhusiana na Azimio hilo ambayo yalijibiwa na Mwalimu Nyerere mwenyewe kama ilivyo katika kijitabu hiki. Madhumuni ya kuchapisha kijitabu hiki ni kuwakumbusha vijana wetu historia ya Azimio na kuibua mjadala kuhusu mazingira ya leo na somo gani tunaweza kujifunza.